kwa nini usiogope?
Ayu
3:25 maana jambo hilo nichalo hunipata, nalo unitialo hofu
hunijilia.
HOFU NI UTUMWA
Rum 8:15 kwa kuwa hamkupokea tena
roho wa utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambayo kwa
hiyo twalia Aba yaani Baba.
2 TIM1:7 Maana Mungu hakutupa
roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.
HOFU INA ADHABU
1 Yoh 4:18 katika pendo hamna
hofu ; lakini pendo lililo kamili huitupa nje hofu, kwa maana hofu ina adhabu
na mwenye hofu hakukamilishwa katika pendo.
HOFU INA ADHABU MAAMUZI YOYOTE YANAYOAMULIWA KATIKA HOFU
YANAGHARIMU.UKIKAA KATIKA HOFU UTAKUW UNATEKELEZA ADHABU.
KATAA HOFU
kataa hofu maana Mungu ameweka
nguvu ndani yako huna sababu ya kuogopa maisha, kwamba watakuonaje
usipofanikisha mpango ulioanzisha, hofu ya kuachika hivyo unatenda dhambi ili
usiachike n.k .Yaliyokuwako yamekuwako hivyo uwezi kubadilisha kitu cha msingi
jitiishe kwenye mikono ya Mungu ili uwe salama.
MAOMBI
1. Nakataa kuogopa kwa sababu
Mungu hakunipa roho ya woga bali ya
nguvu, na ya upendo na ya moyo wa kiasi katika Jina Yesu.
2. nafunga Roho YA hofu kwenye
maisha yangu katika jina la Yesu.
3. kila nguvu nyuma ya kila
kitendo cha hofu maishani mwangu ipigwe kwa hasira ya Mungu.
4. kila kitu ninachokiogopa
naamuru kisinijilie (kataa kisikutokee) sasa katika jina la Yesu.
kila nilichowahi kukiogopa
hakitanitokea katika jina la Yesu.
Post a Comment