. |
Taarifa ya mdhibiti na mkaguzi wa hesabu za serikali kuhusiana na kashfa ya wizi wa bilioni 321 kwenye akaunti ya tegeta Escrow iliyokabidhiwa kwa katibu wa bunge imekutwa inasambazwa mitaani huku ikiwa imenyofolewa kurasa tatu za mwisho zenye majina ya waliohusika na mgawo wa fedha hizo kwa lengo la kutengeneza propaganda ili kuwadanganya wananchi kuwa taarifa hizo hazijawataja wahusika.
Akizungumza na waandishi wa habari mwenyekiti mwenza wa ukawa Mh.
James Mbatia amesema zipo taarifa za baadhi ya waliokuwa wanasambaza
taarifa hizo kuwa wamekamatwa na jeshi la polisi na kuwataka wananchi
kutoa taarifa kituo cha polisi ili waweze kuchukuliwa hatua haraka
ambapo amesesistiza kwamba (UKAWA) wanataka taarifa hiyo iwasilishwe
bungeni kwa ajili ya kujadiliwa Jumatatu .
ITV imemtafuta kamanda wa polisi mkoa wa dodoma David Misime na
katibu wa bunge Dr.Thomas Kashilillah ambao wamesema nao wanazisikia
taarifa hizo na wanazifanyia kazi ili kutoa taarifa yao.
source ITV
Post a Comment